Kuendeleza Uhuru wa Vyombo vya Habari ni Kudumisha Demokrasia ya Kenya
Published Jul. 18, 2024
00:00
00:00

Kukamatwa kwa mwanahabari mtajika Macharia Gaitho katika mazingira ya kudhalilisha na kuhujumu haki za mtu, siku moja tu baada ya mwanahabari wa Kameme kufyatuliwa risasi na polisi huko Nakuru alipokuwa akiangazia maandamano dhidi ya serikali kunaonesha kuchipuka tena kwa majaribio ya kudunisha uhuru wa vyombo vya habari unaolindwa Kikatiba. Kamwe tusikubali hilo kufanyika, uhuru wa wanahabari na vyombo vya habari ni mhimili muhimu mno wa demokrasia ya Kenya.