Dhuluma Dhidi ya Uhuru wa Habari
Published Jul. 17, 2024
00:00
00:00

Tukio la kufyatuliwa risasi mwanahabari wa Kituo cha Kameme Nakuru Wanjeri wa Kariuki katika maandamano dhidi ya serikali ni mfano hai wa majaribio ya serikali kuwalenga wanahabari, kwa lengo la kuwanyamazisha wasitekeleze wajibu wao ambao unalindwa na Katiba ya Kenya. Kamwe hatuko tayari kurudisha nyuma hatua kubwa zilizopigwa katika kukuza demokrasia na kudumisha uhuru wa vyombo vya habari.