Wakati mwanasiasa Karisa Nzai Munyika alipoanza kumvizia mbunge wa Malindi miaka ya 2000s, alijiua wazi Aisha Jumwa Karisa siyo mtu wa kuraukia. Wote walipatana wakiwa wanasisasa, bwana akiwa diwani wa Manispaa ya mji wa Mombasa na mke akiwa diwani wa Takaungu, baraza la mji wa Kilifi .
Mke akiwa diwani, alibahatika pia kuchaguliwa kama mwanamke wa kwanza kuwa mwenyekiti wa baraza la mji wa Kilifi. Bwana naye akaishia kuwa naibu wa Meya wa Mombasa kabla ya zunguluke ya maisha kuwageukia miaka ya 2013-2014.