Inspekta Mkuu wa Polisi, Hillary Mutyambai ameagizwa kumpa ulinzi Seneta wa Kakamega, Cleophas Malala kufuatia madai kwamba maisha yake yamo hatarini.
Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Sheria na Usalama katika Seneti, Yusuf Haji amesema madai yaliyoibuliwa na Malala yana uzito hivyo basi anapaswa kupewa ulinzi haraka iwezekanavyo.