Serikali, mashirika ya Umoja wa Mataifa UN na yale ya kutetea haki za kibinadamu yametakiwa kuchukua hatua madhubuti kuendeleza na kuwekeza katika usaidizi wa kisaikolojia kwa watu walioathiriwa na mizozo ya kivita.
Shirika la Human Rights Watch linasema idadi kubwa ya watu walioathirika kiakili mwaka huu inatokana na mizozo ya kijamii na vita pamoja na hali ngumu ya kimaisha kufuatia ukame na baa la njaa.