29th November, 2019
Halmashauri ya ndege nchini KCAA sasa imepewa idhini rasmi kutoka kwa hazina ya fedha nchini sawa na kitengo cha huduma za umma kuajiri takriban wafanyakazi mia tatu wakiwemo wahudumu wa ndege, maafisa wa kutoa vibali sawa na wale wa ukaguzi wa huduma za ndege. Haya yanajiri wakati ambapo halmashauri hiyo imekuwa ikiyumbayumba kutokana na uhaba wa wafanyakazi.hata hivyo kuhusiana na kisa cha abiria mmoja aliyeanguka nchini London kutoka kwenye ndege iliyokuwa ikitoka kwenye uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta halmashauri hiyo imejitenga na uchunguzi unaondelea kuhusiana na tukio hilo ambali lingali kitendawili wakisema kwamba hawamo miongoni mwa wanaendeleza uchunguzi huo.