17th September, 2018
Jumuia ya afrika mashariki imekariri umuhimu wa kuhifadhi msitu wa mau, kama juhudi mojawapo ya kuhifadhi mto mara, unaotegemewa sana na watu wapatao milioni moja nukta mbili, katika mataifa ya Kenya na Tanzania. aidha maji ya mto mara ni muhimu kwa wanyama pori katika mataifa hayo mawilihaya yalidokezwa kwenye sherehe za mto mara, makala ya saba, sherehe zilizofanywa huko kilgoris. katika hafla hiyo, maazimio ya kuuhifadhi msitu wa mau yalipitishwa kwa kauli moja, huku katibu wa tume ya ustawi wa ziwa victoria ali matano na katibu katika wizara ya maji simon chlagui wakiwakilisha kenya; Tanzania ikiwakilishwa na naibu waziri wa maji juma aweso.