30th September, 2020
Wahudumu wa bodaboda katika kaunti ya Busia wamelalamikia ongezeko la visa vya ajali barabarani zinazosababishwa na wanafunzi wa shule wanaodaiwa kujiingiza kwenye sekta ya uchukuzi msimu huu wa Korona. Wakizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa afisi mpya ya chama chao katika eneo la Ojamii eneo bunge la Teso kusini kaunti ya Busia, wahudumu hao wamesema kuwa wanafunzi wamesajili idadi kubwa ya ajali zinazohusiana na pikipiki kwani wengi wao wanaziendesha bila kuzingatia sheria za barabarani. Kupitia kwa viongozi wao,wahudumu hao wamesema kuwa zaidi ya wanafunzi mia moja wanauguza majeraha ya mwili baada ya kuhusika kwenye ajali za barabarani tangu shule zifungwe mwezi machi mwaka huu,huku wakitaka vitengo husika kuingilia kati na kuwachukulia hatua kali wanaojihusisha.