30th September, 2020
Kenya inakumbwa na upungufu wa maziwa wakati uzalishaji wake umepungua kutokan na sababu za hali ya anga, gharama ya uzalishaji na hata mbinu za uimarikaji wa Ng’ombe. Kulingana na mtafiti wa maziwa katika shirika la serikali la KALRO, Daktari Tobias Onyango, wakulima wa maziwa nchini, huzalisha maziwa ambayo hayafiki mahitaji ya kitaifa. Kwa sasa ni kaunti 24 pekee zilizojikita katika kilimo cha maziwa ambazo pia zinakabiliwa na chungu nzima ya changamoto ikiwemo malisho finyu, magonjwa, ukumbatiaji finyu wa teknolojia na gharama ya juu ya bidhaa za uvunaji shambani. Daktari Onyango ameyazungumza hayo kwenye warsha ya mafunzo ya wiki mbili katika taasisi ya mafunzo ya kilimo kaunti ya Kitui kwa maafisa wa mifugo kutoka kaunti za Kajiado na Taita Taveta