23rd September, 2020
Wabunge waliopo kwenye kamati ya kusimamia pesa za Usawi wa maeneo bunge ( CDF) wameikosoa serikali kwa mipangilio ya kufungua shule wakati huu. Wabunge hao walizungumza huko Embakasi kwenye ukaguzi wa miradi ya hazina ya CDF, wakisema kwamba serikali inajitia hamnazo kuhusu ukosefu wa miundomsingi inayohitajika kupambana na msambao wa homa ya Korona.