.
23rd September, 2020
Shirika la Wanyama Pori KWS liko mbioni kuwaokoa wanyama pori waliokwama katika kisiwa cha Longcharo katika Ziwa Baringo. Wanyama hao wakiwemo Ngiri, Swara na Twiga walijipata pabaya baada ya viwango vya maji kuongezeka na kukifanya kisiwa hicho ambacho kimekuwa makazi yao kwa zaidi ya mwongo mmoja kuwa finyu.