.
21st September, 2020
Walimu kote nchini wameombwa kuripoti kazini jumatatu Sept, 28 kwa maandalizi ya ufunguzi wa shule. Afisa mkuu wa tume ya huduma za walimu tsc, nancy Macharia na waziri wa elimu prof george magoha walitoa tangazo hilo mapema leo baada ya kupokea ripoti kutoka kwa jopokazi lililopewa jukumu la kuandaa mchakato wa ufunguzi wa shule baada ya jinamizi la korona. Hata hivyo Tarehe ya ufunguzi bado haijatangazwa.