18th September, 2020
Mbunge wa Emurua Dikirr johana Ng’eno atafikishwa mbele ya kamati ya nidhamu ya chama cha kanu kuhusiana na matamshi yake yaliyotajwa kama ya matusi. Katibu mkuu wa chama hicho Nick Salat amesema kuwa walikuwa wamepewa ruhusa kumfikisha kiongozi huyo mbele ya kamati hiyo na viongozi wa eneo hilo waliofika huko kuzungumza na kiongozi wa chama hicho seneta Gideon Moi. Kwa upande wake, Seneta Moi alizitaka jamii hizo kuishi kwa amani akiongeza kuwa serikali inafanya juhudi zote kuhakikisha kuwa suluhu ya kudumu inapatikana.