16th September, 2020
Makundi ya kina mama pamoja na vijana kutoka pembe tofauti za Kaunti ya Nairobi yanatarajiwa kunufaika na zaidi ya Shilingi Milioni Hamsini zilizotolewa na Wizara ya Vijana na jinsia ili kuwainua kibiashara .Akizungumza kwenye hafla ilioandaliwa katika makao makuu ya shirika linaloshughulikia maslahi ya watu wanaosihi na ulemavu APDK hapa Nairobi katibu mwandamizi katika wizara hiyo Rachael Shebesh amesema ufadhili huu utawasaidia akina mama pamoja na vijana kujiendeleza kiuchumi baada ya biashara zao kuathirika kutoka na janga la Korona. Mbunge wa Westlands Tim Wanyonyi vile vile amewataka akina mama kuwa mstari wa mbele kujisajili kwenye mashirika ya hazina na mikopo kwa ajili ya kujiendeleza katika shughuli za kibiashara