.
16th September, 2020
Jopo la Maseneta 12 ambalo limepewa jukumu la kutafuta muafaka kuhusu suala nyeti la Ugavi wa Fedha kwa Serikali za Kaunti litaanza vikao vyake rasmi kesho kutathmini ahadi ya Rais Uhuru Kenyatta ya kuongeza mgao huo kutoka shilingi billion 316 hadi shilingi bilioni 366 mwaka ujao wa matumizi ya Fedha. Jopo hilo limeahidi kuweka bidii ili kusuluhisha mgogoro huo. Bunge la taifa sasa litawajibika kuweka ahadi ya Rais kwenye sheria ya Ugavi wa Fedha kati ya serikali ya taifa na zile za kaunti, almaarufu division of revenue act, ili kutimiza ahadi ya serikali kwa magatuzi.