.
16th September, 2020
Waziri wa elimu Prof George Magoha amekariri kuwa hana mamlaka ya kuamuru ni lini taasisi za masomo zitafunguliwa ila mamlaka hayo ni ya wataalamu wanaoshughulikia suala hili. Magoha alizungumza kwenye shule ya upili ya Kapsisiywa Kaunti ya Nandi wakati wa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa maktaba ya kisasa itakayogharimu kima cha shilingi Milioni 100, mradi unaofadhiliwa na mwanariadha maarufu Eliud Kipchoge. Magoha ameendelea kulaumu vyombo vya habari kwa kile ametaja ni kutoa habari za kukanganya.