2nd September, 2020
Waziri wa usalama wa ndani Daktrai Fred Matiang’i ametoa orodha ya watu tisa wanaoshukiwa kufadhili kundi la kigaidi la Alshaabab. Waziri Matiang’i ameamuru kugandisha kwa mali na fedha ya wahusika hao ambao ni halima adan ali, Waleed Ahmed Zein, Sheikh Guyo Gorsa Boru, Mohammed Abdi Ali (Abu Fidaa), Nuseiba Mohammed Haji, Abdimajit Adan Hassan, Mohammed Ali Abdi, Muktar Ibrahim Ali na Mire Abdullahi Elmi. Aidha Matiang’i ameelezea kuwa serikali itaendelea kumulika shughuli za Ugaidi kama njia mojawapo ya kupiga vita na pia kuwanasa wahusika. Orodha hii imetolewa miaka saba baada ya wanamgambo wa Alshaabab kuvamia duka kuu la Westgate hapa jijini Nairobi kuwaua watu zaidi ya siti na saba. Hata hivyo serikali haikutaja namna na njia wahusika hao tisa walifadhili kundi hilo la Alshaabab.