12th June, 2020
Mwenyekiti wa chama cha wanasheria nchini tawi la nairobi
eric theuri amemtaka rais uhuru kenyatta kuwa katika
msitari wa mbele kwa kuheshimu sheria na maagizo ya
mahakama ili kuweka imani ya wananchi kwenye mahakama.
wanasheria hao wameunga mkono shinikizo la jaji mkuu
david maraga la kumtaka rais uhuru kenyatta kuwateua
maramoja majaji 41 waliopendekezwa na tume ya kuajiri
maafisa kwenye idara ya mahakama, jsc. Theuri alimshutumu
mkuu wa sheria kihara kariuki kwa kumpotosha rais na
kujaribu kuteka mahakama.