14th May, 2020
Jamaa mmoja katika kijiji cha Emusioma kaunti ya Kakamega anaishi na masaibu miaka 15 baada ya kumkabidhi nduguye moja ya figo zake alipopatwa na maradhi ya figo.
Nduguye aliitumia figo hiyo kwa miaka kumi kabla ya kufariki. Sasa ikidaiwa nduguze wanataka kumtimua kutoka kwa shamba la familia kwa madai alipewa zawadi ya shamaba jingine na marehemu kama shukrani ya kumpa figo.