2nd October, 2018
Baada ya kuwa rumande nchini Tanzania kwa zaidi ya miaka mitano unusu bila kufunguliwa mashtaka hatimaye Mkenya Don Bosco Gichana ameachiliwa huru. Bosco ambaye alitiwa mbaroni mwaka wa 2013 kwa tuhuma za uhaulishaji wa fedha kutoka kwa raia wa Marekani waliostaafu aliachiliwa mapema hivi leo na akarejea nchini kupitia kivuko cha mpakani cha Namanga. Kosa hilo hata hivyo lilimgharimu Bosco faini ya shilingi milioni kumi na tano. Kwenye kampeni za uchaguzi wa mwaka wa 2007 Gichana aligonga vichwa vya habari baada ya kumtunuku kiongozi wa ODM Raila Odinga gari jekundu aina ya hammer ambalo lilikuwa na umaarufu mkubwa wakati wa kampeni za kisiasa.