1st October, 2018
Mke wa mbunge wa Nakuru Town East David Gikaria Bi Violet Nzisa amefikishwa mbele ya mahakama ya Nakuru kujibu mashtaka ya kuidharau mahakamani. Hii inafuatia agizo la mahakama la kumtaka arejee mahakamani baada ya kauchiliwa kwa dhamana ya shilingi laki moja. Inaarifiwa kuw abi nzisa alipuuza agizo la mahakama la kumtaka alipe mwathiriwa wa ajali zaidi ya shilingi laki saba mwaka uliopita baada ya kumngonga kwa gari.