3rd September, 2018
Chifu wa zamani aliyewezesha kunaswa kwa mshukiwa mkuu wa uhalifu na visa vya mauaji katika eneo la mlima Elgon Timothy Kiptanui Kitai, maarufu Cheparkach yuko kwenye njia panda kuhusu zawadi ya shilingi milioni moja iliyoahidiwa na serikali kwa mtu yeyote ambaye angetoa habari ambazo zingewezesha kukamatwa kwa mshukiwa huyo. Wakaazi walioshuhudia cheparkach akikamatwa na chifu huyo wa zamani na kisha kuwasilishwa katika kituo cha polisi sasa wanasema kuwa huenda kuna njama ya baadhi ya maafisa serikalini kutaka kumnyima chifu huyo zawadi anayostahili kupokea baada ya kuisadia serikali kumnasa mhalifu.