Mawakili wanaowakilisha wakili Willie Kimani wataka mto wa Oldonyo Sabuk upewe ulinzi
12th July, 2016
Mawakili wanaowakilisha wakili Willie Kimani, mteja wake Josephat Mwenda na dereva Joseph Muiruri waliouawa hivi majuzi wametoa ombi kwamba mto wa Oldonyo Sabuk upewe ulinzi hasa kwa kuwa maiti zao zilipatikana humo. Maswali pia yameibuka kuhusu walipokuwa polisi wakati kundi la waandamanaji liliteketeza kituo cha Syokimau. Hayo yameibuka kwenye kesi inayoendelea ya mauaji hayo. Nick Wambua anaarifu