Buriani ya Mama Lucy Kibaki yafanyika Othaya katika Kaunti ya Nyeri
7th May, 2016
Mama Lucy Kibaki amezikwa hii leo nyumbani kwake katika Kaunti ya Nyeri huku Maelfu ya waombolezaji wakihudhuria ibada yake ya wafu. Rais Uhuru Kenyatta aliongoza ujumbe wa serikali ya Kenya sawa na Rais Mustaafu wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete aliyesoma salamu za rambirambi kutoka kwa Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli. Wanenaji wakiwemo watoto wa Mama Lucy walimsifia kwa kulinda familia yake na Rais Mustaafu Mwai Kibaki. Mwanahabari Carol Nderi ametuandalia taarifa ifuatayo.