Babu Owino afikishwa mahakamani kwa mashtaka ya kumdhulumu mshindani wake Mike Jacobs
5th May, 2016
Babu Owino, mwenyekiti wa chama cha wanafunzi wa chuo kikuu cha Nairobi, SONU, amefikishwa mahakamani kujibu mashtaka ya kumdhulumu mshindani wake wakati wa kampeni za SONU Mike Jacobs. Owino alifika kwenye mahakama ya Kibera asubuhi akiwa na mawakili watatu baada ya kuzuiliwa usiku kucha katika kituo cha polisi cha Kilimani. Alikanusha mashataka hayo na kuachiliwa kwa dhamana ya shilingi laki moja pesa taslimu. Aidha, mahakama ilimtaka kutoa anwani ya mtu atakayewasiliana nayo iwapo Owino hatapatikana. Owino alichaguliwa tena kwenye kura tata za SONU zilizosababisha kufungwa kwa muda kwa chuo hicho, huku wanafunzi waliohusishwa na vurugu hizo wakitimuliwa