Gor Mahia yalaza Bandari, Ulinzi yasajili ushindi dhidi ya Chemilil Sugar
28th April, 2016
Gor Mahia imeendeleza msururu wake wa matokeo mema katika ligi kuu nchini baada ya kulaza Bandari 2-0 katika mechi ya ligi kuu nchini huku kikosi cha Ulinzi kikisajili ushindi wa 2-1 dhidi ya Chemilil Sugar. John Makwata alikuwa wa kwanza kucheka na wavu katika dakika ya 32 hii ikiwa ni kabla ya Hillary Echesa kuwasawazishia Chemilil Sugar. Bao la pili na la ushindi kwa ulinzi likawa ni lake John Makwata kupitia kwa penalty. Katika mechi tofauti, bandari ilikosa kumakinika na kupata kichapo cha 2-0 huku George Odhimba akifunga la kwanza naye Felly Mulumba akajifunga na kumaliza mechi 2-0. Sonny sugar ikalaza kakamega Homeboyz 1-0 Posta Rangers nayo ikatwaa alama tatu baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Ushuru na mechi ya Tusker dhidi ya Mathare United ikakamilika 2-2