Gwiji wa Nyimbo za Lingala Papa Wemba afariki Mjini Abidjan
24th April, 2016
Mashabiki wa miziki ya kale kama vile rhumba na lingala wanazidi kuomboleza baada ya gwiji wa miziki hiyo papa wemba kufariki. Papa wemba alianguka na kuzirai alipokuwa akitumbuiza mashabiki wake katika mji mkuu wa Ivory Coast, Abidjan. Papa wemba ambaye jina lake halisi ni shungu wambadio alikuwa na miaka 66. Miziki yake iliyovuma inajumuisha yolele na show me the way.