Bei ya petroli yashuka kote nchini
14th April, 2016
Bei ya petroli imeshuka kote nchini . Hii ni baada ya tume ya kuthibiti kawi ERC kutangaza mabadiliko katika bei za mafuta kote nchini . Bei ya mafuta ya petroli imeshuka kwa shilingi 4 na senti 87 na kuwa shilingi 80.71 kwa lita moja jijini nairobi ilhali dizeli ikiwa imepanda kwa senti 53 . Bei ya mafuta taa imepanda kwa shilingi moja na senti 81 . Bei hizo zitaanza kutekelezwa kutoka kesho tarehe 14 hadi tarehe klumi na nne mwezi wa Mei .