Abiria wanne wafariki katika ajali ya barabarani katika eneo la Murang'a
14th April, 2016
Abiria wanne wamefariki katika ajali ya barabarani usiku wa kuamkia leo baada ya gari lao kugongwa na lori lililokuwa limebeba mbolea karibu na chuo cha walimu cha Murang`a. Akithibitisha kisa hicho OCPD wa eneo hilo samuel kosgei amesema kuwa wanne hao ambao ni wanawake walikuwa wakitoka katika mazishi katika eneo la meru ilhali lori lilikuwa likielekea nanyuki. Watu wawili akiwemo dereva wa gari hilo walinusurika na sasa wanapokea matibabui katika hospitali ya thika level five. Wanaotumia barabara ya kenol – makuyu wameombwa kuwa waangalifu kupunguza ongezeko la ajali .