Wafanyabiashara wanaotengeneza maziwa gushi ya yoghurt kutumia kemikali wanaswa Nakuru
11th April, 2016
Mtazamaji iwapo una uraibu wa mtindi au yoghurt ukipenda yafaa sasa uanze kutahadhari kila unaponunua maziwa hayo yaliyoganda… hii ni baada ya wizara ya afya ya umma kuwanasa wafanyabiashara katika kaunti ya Nakuru wanaotengeneza maziwa haya ila hawatumii hata tone la maziwa haswa. Inaarifiwa wamekuwa wakichanganya kemikali kupata mchanganyiko unaotoa ladha ya maziwa.