Wakaazi wa Mandera washerehekea maadhimisho ya tatu ya ugatuzi
27th March, 2016
Wakaazi wa kaunti ya Mandera wakishirikiana na serikali ya kaunti hiyo walisherekea maadhimisho ya tatu ya ugatuzi ya kaunti hiyo. Kaunti ya mandera ni kaunti ambayo imekabiliwa na visa vya mashambulizi ya kigaidi visa ambavyo vimetishia maendeleo ya kaunti hiyo. Licha ya changamoto za ukosefu wa usalama zinazoshuhudiwa katika kaunti hiyo wakaazi wanasema kuwa huu ndio mwamko mpya wa kaunti hiyo.