Kiongozi wa kanisa la Kiangalikana Eliud Wabukhala awataka Wakenya wajiepushe na ukabila
27th March, 2016
Kiongozi wa kanisa la kiangalikana nchini Kenya Eliud Wabukhala anawataka Wakenya kujiepusha na ukabila na desturi zote ambazo zinaweza kuleta mgawanyiko katika nchi hasa katika uchaguzi mkuu ujao wa 2017. Askofu huyo mkuu ambaye anatakiwa kustaafu katikati ya mwaka huu vile vile aliwataka wanasiasa kustaarabika na kujiepusha na matamshi ya chuki ambayo yanaweza kuleta uchochezi nchini.