Utafiti mpya wa Infotrak: Rais Uhuru Kenyatta aongoza kwa asilimia 45
27th March, 2016
Endapo uchaguzi ungeitishwa sasa hivi Rais Uhuru Kenyatta angechaguliwa kwa wingi wa kura . Utafiti uliofanywa na shirika la Infotrak unaonyesha kuwa Rais Uhuru Kenyatta anaongoza kwa asilimia 45 dhidi ya kinara wa CORD Raila Odinga akiwa na asilimia 28. Mrengo wa Jubilee umeonekana kuimarika zaidi ukipata asilimia 40% ikilinganisha na mwaka jana ambapo umaarufu wake ulikuwa asilimia 37. 5.