Waziri Najib Balala afungua Mbuga ya Rimoi
19th March, 2016
Waziri wa utalii Najib Balala ametoa wito kwa wakenya kuwa mstari wa mbele kuuza vivutio vya kitali vya humu nchini kimataifa. Balala alisifia hususan uwezo wa maeneo kama ya bonde la ufa kujitokeza kama nguzo ya utalii nchini iwapo jamii za maeneo hayo zitaungana kubuni mazingira mwafaka ya uwekezaji. Alizingumza kwenye Kaunti Ya Elgeyo Marakwet wakati wa uzinduzi wa mbuga ya wanayama ya kitaifa ya rimoi. Mbuga hiyo inajivunia kuwa na ndovu wakubwa zaidi ulimwenguni ambao idadi yao ni zaidi ya mia sita. Kaunti hiyo imewekeza shilingi milioni 20 kuimarisha mbuga hiyo.