Mashindano za Gofu kuanza Machi 15
10th March, 2016
zimesalia siku saba tu kabla ya makala ya mwaka huu ya kinyanganiro cha gofu almaarufu Barclays Kenya Open kungoa nanga. Mashindanoi hayo yataandaliwa kati ya tarehe 17 na 20 ikiwa ni baada ya michuano ya chipukizi pamoja na magwiji yatakayoandaliwa tarehe 15 na 16. Mshindi atatia kibindoni takriban shilingi milioni 25 huku washindani 156 wakitarajiwa kushiriki. Vigogo 100 wanaoshiriki katika msururu wa bara ulaya ni miongoni mwa watakaoshiriki huku wengine hamsini wakitoka katika mataifa tofauti ya afrika. Kampuni ya coca-cola imetoa ufadhili wa takriban shilingi milioni 15 zitakazotumika katika mandalizi ya mashindano ya chipukizi pamoja na wachezaji wenye uzoefu siku ya jumanne tarehe 15.