Chuo cha Kabarak,Maseno,Alliance na Kahuhia zafana katika mtihani wa KSCE 2015
3rd March, 2016
Shule ya upili ya Moi Kabarak huenda ikawa ndiyo bora zaidi kwenye mtihani wa mwaka jana ambapo zaidi ya wanafunzi 200 wamejinyakulia alama ya A. Aidha kwenye orodha ya wanafunzi 15 bora nchini wanne kati yao ni wa shule hiyo. Shule zingine zenye wanafunzi bora miongoni mwa 15 bora ni Alliance yenye wanafunzi watatu miongoni mwa 15 bora, Kahuhia girls mwanafunzi mmoja, Kapsabet boys huko nandi mwanafunzi mmoja, Maseno kutoka Kaunti ya Kisumu wanafunzi watatu,Moi girls kutoka Kaunti ya Uasin Gishu mwanafunzi mmoja pamoja na shule ya wamy kutoka Kaunti ya Nairobi.