Wachezaji chini ya miaka 12 kufunzwa chini ya mradi wa sports for tomorrow
20th February, 2016
Shule hamsini kutoka eneo la Eastlands mjini Nairobi zitanufaika na mradi wa sports for tomorrow ambao utatumika kwa ajili ya kuwapa chipukizi kutoka maeneo hayo nafasi ya kujifunza mchezo wa tenis. Hii ni baada ya chuo cha michezo cha Tsakuba kutoka Japan kutia mkataba na mathare youth na shirikisho la tennis nchini ktta. Mkataba huo utawasaidia wasichana walio chini ya umri wa miaka kumi na mbili ambao watapewa mafunzo na makocha kutoka maeneo mbalimbali.mwenyekiti wa shirikisho la tennis nchini Andrew Mudibo alidokeza kwamba mradi huo ni njia moja ambayo shirikisho hilo linatumia kukuza mchezo huo nchini.