Wakfu wa Wings To Fly yahimiza jamii kufadhili wanafunzi waliokosa karo
3rd February, 2016
Zaidi ya wanafunzi 200 waliopata alama za juu kwenye mtihani wa KCPE maeneo ya Ruiru, Juja na Thika wana changamoto ya kujiunga na shule za upili kutokana na ukosefu wa karo. Baadhi ya wafadhili kutoka kwa wakfu wa Wings To Fly unaoongozwa benki ya Equity wametoa wito kwa jamii kuwafadhili wanafunzi hao ili wasikose elimu.