Mugabe ataka Afrika ishirikishwe kwa baraza la usalama
30th January, 2016
Rais wa Zimbabwe ambaye pia ni mwenyekiti wa umoja wa Afrika ametoa wito kwa umoja wa mataifa kujumuisha mataifa ya afrika katika baraza la usalama la umoja wa mataifa. Mugabe amesema kuwa mataifa ya bara afrika yanafaa kujiondoa katika umoja wa mataifa iwapo yataendelea kutengwa na kukosa kuhusishwa katika maamuzi ya maana kwenye umoja huo. Mugabe amesema hayo akifungua kikao cha marais na viongozi wa mataifa wanachama wa umoja wa afrika mjini Addis Ababa Ethiopia.