Washukiwa wa wizi waokolewa na polisi baada ya kufumaniwa na wakaazi wakiiba pombe Kakamega
28th December, 2015
Polisi wa utawala waliwazuia wakaazi wa Khayega, kaunti ya Kakamega kuwapiga washukiwa watatu wa wizi baada ya kuwafumania wakiiba katika duka moja la kuuza pombe. Wakaazi wanadai wezi hao walikuwa wamepora duka hilo la ingo jana usiku na waliporudi kwa mara ya pili, walishindwa kutimiza nia yao.