Makao ya watoto yatima yageuka mahala pa dhuluma za kimapenzi na ubakaji
29th November, 2015
Mtazamaji taarifa ifuatayo ni ya kuvunja moyo, ambapo makao yaliyokusudiwa kuwa hifadhi ya watoto yatima yamegeuka na kuwa mahala pa dhuluma za kimapenzi na ubakaji. Jamaa mmoja katika kitongoji cha Kayole anadaiwa kumbaka msichana wa umri wa miaka kumi na saba katika makao yake ya watoto kwa mwaka moja sasa. Na kama anavyoarifu Geff Kirui licha ya kisa hicho kuripotiwa, mshukiwa alikamatwa na kuachiliwa siku chache baadaye. Hata hivyo jioni ya leo kwa njia ya simu OCPD wa Kayole ali nuno amearifu KTN News kuwa mshukiwa anasakwa na tayari idhini imetolewa kwa OCS kuvunja lango la nje la kituo hicho baada ya kubainika kuwa bado kuna watoto humo ndani licha ya amri kutolewa ya kukifunga kituo hicho.