Hatimaye waziri wa ugatuzi Bi Anne Waiguru ajiuzulu kufuatia shinikizo za Wakenya
21st November, 2015
Shinikizo za Wakenya zilidhihirika wazi na kumpelekea waziri wa ugatuzi na mipango ya taifa Anne Waiguru kujiondoa afisini. Kwenye mkutanon na wanahabari mapema alasiri ya leo, Waiguru ametaja hali yake ya afya kama sababu kuu ya kujiuzulu baada ya kushauriwa na daktari wake. Shinikizo za Waiguru kujizulu zilianza pale alipoeleza kuwa shilingi milioni 791 zilipotea katika wizara yake, chini ya mpango wa taifa kwa vijana NYS.