John Pombe Magufuli wa CCM ndiye rais mteule wa Tanzania baada ya kumpiku Edward Lowassa wa Chadema
29th October, 2015
Habari kutoka Tanzania ambapo tume ya uchaguzi nchini humo imemtangaza John Pombe Magufuli , wa CCM kuwa mshindi wa uchaguzi mkuu uliofanyika siku Ya jumapili. Tume hiyo imesema Magufuli amejinyakulia zaidi ya kura milioni nane huku mshindani wake Edward Lowasa wa chama cha Chadema akiwa na kura zaidi ya milioni sita. Hata hivyo upinzani umeyapinga matokeo hayo licha ya kuwa katiba ya Tanzania hairuhusu mlalamishi kuwasilisha rufaa mahakamani kupinga matokeo ya urais.