Waziri wa elimu Jacob Kaimenyi akiri kuwa angali na imani na baraza la mitihani KNEC
27th October, 2015
Waziri wa elimu Jacob Kaimenyi amekiri kuwa angali na imani na baraza la mitihani humu nchini - KNEC..akiwa mbele ya kamati ya bunge kuhusu elimu kaimenyi alisisitiza haya licha ya yeye na washikadau kukubali kuwa kumekuwepo na changamoto ya wizi wa mitihani. Wakati huo huo mbunge wa mbooni kisoi munyao amewasilisha hoja bungeni ya kutaka baraza la KNEC kuvunjiliwa mbali kwa kushindwa kusimamia mtihani ipasavyo. Francis Mtalaki na maelezo zaidi.