Watu kadhaa wajeruhiwa kwenye mkanyagano uliozuka katika Chuo cha Bandari
5th July, 2015
Watu kadhaa wamejeruhiwa kwenye mkanyagano uliozuka katika chuo cha bandari , mjini mombasa wakati wa shughuli ya usajili wa wafanyakazi bandarini. Mkanyagano huo unadaiwa kuanza wakati polisi walipojaribu kutawanya kundi la watu lililokuwa likisumakana kuingia kwenye chuo hicho kushiriki kwenye shughuli hiyo ya usajili. Iliwalazimu maafisa wa polisi kurusha vitoa machozi ili kutawanya umati uliokuwa umekusanyika hapo.