SIKU YA KINA MAMA DUNIANI: Jamii yapewa hamisisho la maradhi ya Lupus
10th May, 2015
Wakenya wanaoathirika na ugonjwa wa Lupus walijiunga na wengine kote duniani kusherekea siku ya wagonjwa wa maradhi hayo. Ugonjwa huo umetajwa kutoeleweka pakubwa na wengi kwani huathiri pakubwa viungo vingi vya mwili. Wagonjwa wa maradhi haya pia wamelalamikia kuhusu kuwepo kwa viwango vya juu vya unyanyapaa, hata hivyo kumekuwepo na kampeini za kuwahudumia wagonjwa hao humu nchini.