Mkurugenzi mkuu wa NEMA asema tume hiyo haina uwezo wa kufuatilia kila kinachoendelea viwandani
6th May, 2015
‘’hatuna uwezo wa kufuatilia kila kinachoendelea katika viwanda mbali mbali vya humu nchini’’ hii ndio kauli ya geoffrey wahungu ambaye ndiye mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya kitaifa yanayosimamia mazingira nema baada ya kufika mbele ya kamati ya bunge kuhusu mazingira hii leo. Wahungu alitakiwa kuieleza kamati hiyo wajibu wao kuhusiana na uchafuzi wa mazingira uliotekelezwa na kiwanda cha kutengeneza madini aina ya lead katika kitongoji cha owino -uhuru mjini mombasa.