Chelsea lapata ushindi kwenye dimba la capital one
2nd March, 2015
Jose Mourinho alitwaa taji lake la kwanza baada ya kurejea kuongoza klabu ya Chelsea huku akilaza Tottenham Hotspurs mabao 2-0 hapo jana. Mabao ya nahodha wa timu hiyo John Terry na Diego Costa yalikuwa tosha kwa timu hii kutwaa ushindi huo wa dimba la capital one. Ushindi huo ulipokelewa kwa mahanjam na mashabiki wa Chelsea huku kocha wao Jose Mourinho akidokeza kwamba anajihisi kijana barubaru tena. Chelsea iko njiani kutwaa taji la ligi ya uingereza na lile la klabu bingwa ulaya.