Mwekezaji wa kibinafsi avamia ardhi inayohifadhi torathi za kale za jamii ya waswahili
12th January, 2015
Ardhi inayohifadhi torathi za kale za jamii ya waswahili iliyoko eneo la Mtwapa mkabala na ufuo wa bahari sasa inakumbwa na madai ya kunyakuliwa. Maafisa wa makavazi ya Kenya tawi la Pwani wamepinga hatua ya mwekezaji wa kibinafsi kuvamia ardhi hiyo na kuanzisha ujenzi huku akikata miti iliyohifadhiwa kwa karne na karne bila idhini ya makavazi.