Ubishi waongezeka kwenye chama cha UDF baada ya tangazo la kumtimua seneta Khalwale na wengine
27th October, 2014
Chama cha UDF kimewavua uanachama, mwenyekiti wake Hassan Osman, Seneta wa Kakamega Bony Khalwale na Seneta maalum Martha Wangari. Katika kikao maalum cha baraza kuu, hapa Nairobi, wajumbe hao vilevile walipitisha azimio la kubadilisha jina la chama kutoka UDF hadi ANC, likimaanisha Amani National Congress.